WILLIAM MARRION BRANHAM (1909-1965)
William Marrion Branham alikuwa mhubiri wa Biblia mwenye ushawishi mkubwa wa wakati wetu, anayechukuliwa na kuaminiwa na wengi kuwa mwanzilishi wa uponyaji na uamsho ulioanza mwaka 1947.Kuanzia mwaka 1947 hadi wakati
wa kifo chake mwaka 1965, huduma yenye nguvu ya William Branham ilikuwa maarufu
na inachukuliwa kuwa isiyo na kifani katika historia ya mikutano ya Injili. Matokeo
ya huduma ya kimiujiza ya mtu huyu ilitambuliwa si tu Amerika Kaskazini, bali
pia ulimwenguni kote.
Maelfu ya visa
vilivyothibitishwa vya kila namna ya uponyaji vilidhihirishwa katika Marekani,
Kanada, Afrika, na kote ulimwenguni kupitia maombi ya William Branham.
Vipofu walipata kuona,
wagonjwa wa saratani waliponywa, vilema, na wale wasioweza wakaponywa
kabisa. Hakuna ugonjwa uliosimama njiani
kama Mungu alivyothibitisha kwa mamilioni, kwamba Yeye angali ni Mungu leo,
yeye yule jana, leo na hata milele (Waebrania 13:8) katika huduma ya mjumbe
Wake wa wakati wa mwisho kwa wakati wetu.
Lakini muhimu zaidi, William
Branham alituleta Ujumbe wa wakati wa Mwisho uliorejesha mambo yote yaliyokuwa
hayajakamilika katika Biblia ambayo, hata kama vyuo vyote vya Biblia duniani
vingekusanywa pamoja, kamwe visingeweza kutufunulia. Mafundisho haya ni pamoja
na Fumbo la uungu wa Mungu, Ukweli kuhusu Ubatizo kwa Maji, Dhambi ya Asili, Kuchaguliwa
kimbele, Ufunuo wa Mihuri Saba, Kuzaliwa Upya, Alama ya Mnyama, Fumbo la Babeli.
Hizo kweli zimerejeshwa kwa kanisa leo ili kuandaa Bibi wa Yesu Kristo katika kila
taifa kujiandaa kwa Unyakuo, ambao ni kurudi kwa pili kwa Bwana.
William Branham alisema:
“Ama wajiunge na kanisa
langu, ama waanzishe shirika fulani na madhehebu fulani. Sijafanya hivyo kamwe
wala sitafanya hivyo sasa. Sivutiwi na mambo hayo, bali ninavutiwa na mambo ya
Mungu pamoja na watu, na kama naweza kutimiza jambo moja tu nitaridhika. Jambo
hilo moja ni kuona uhusiano wa kweli wa kiroho baina ya Mungu na watu
umeimarishwa, ambapo watu wanakuwa viumbe vipya katika Kristo, wamejazwa na Roho
Wake na wanaishi kulingana na Neno Lake. Ningewaalika, ningewasihi na kuwaonya
watu wote waisikie sauti Yake wakati huu, na kuyatoa maisha yenu kabisa Kwake,
yaani kama vile ninavyoamini moyoni mwangu kwamba nimempa Yeye yote niliyo
nayo. Mungu na awabariki, kuja Kwake na kuifurahishe mioyo yenu.”
MASHAHIDI WA HUDUMA YA BRANHAM.
Zifuatazo ni shuhuda zilizothibitishwa kutoka kwa wahubiri na wainjilisti maarufu duniani kote kuhusu huduma ya William Marrion Branham:
JAMES MORRIS – “Ilikuwa ni Branham,
zaidi ya mwinjilisti mwingine yeyote, aliyeanzisha uamsho na uponyaji mara
baada ya Vita vya pili vya dunia, kufuatia kukutana kwake na malaika mnamo Mei
7, 1946. Neno lilienea kila upande kiasi kwamba aina zote za magonjwa na
mateso yaliponywa papo hapo na yule
mhubiri mdogo wa Indiana. Hata visa vya
kufufua wafu vilichapishwa.” (-The
Preachers)
GORDON LINDSAY – “Hatukuwahi kujua kuhusu
mhubiri yeyote anayeweza kuwaita viziwi, bubu na vipofu awaombee, na kisha kuona
watu hao wakipokea uponyaji mara moja… huduma ambayo ilikuwa zaidi ya yoyote tuliowahi
kuishuhudia hapo awali.” (-The House
that the Lord Built)
TOMMY OSBORN – “Mungu amechagua njia
mbalimbali na za ajabu ili kujidhihirisha Mwenyewe kwa watumishi Wake hasa wale
walioitwa kwa madhumuni maalum, kwa kipindi fulani kama vile wito wa Ndugu
Branham. Kwa ufupi, mtu tunayemjua kama
William Branham alitumwa kuonyesha Mungu tena katika mwili. (-William Branham Memorial Service)
JACK MOORE – ‘Mwenye kipawa zaidi kati
ya wainjilisti wote.’ (-All Things are Possible na David Harell, Jr.)
ORAL ROBERTS – “Mtu mnyenyekevu mwenye
imani kwa Mungu.” (-Healing Waters, Julai 1948)
F.F. BOSWORTH – “Wakati kipawa kinapotenda
kazi, Ndugu Branham ni mtu mwenye ufahamu zaidi wa uwepo na kazi ya Roho
Mtakatifu na ukweli wa kiroho kuliko mtu yeyote niliyemfahamu.” (-A Prophet
Visits South Africa)
GEORGE EKEROTH – “Mungu alimwita mtu
mnyenyekevu huyu na kumtia mafuta kwa huduma yake kwa kiwango ambacho ndani ya
miaka michache fupi jina lake lilijulikana katika vituo vya mbali sana vya
msituni. Popote unapokwenda katika ulimwengu huu, utagundua kwamba jina la mjumbe
huyu limekwisha kutangulia mbele yako.” (-Utangulizi wa Kitabu cha Morris
Cerullo, Wind Over the 20th Century)
GEORGE EKEROTH – “Mungu alimwita mtu huyu
mnyenyekevu na kuipaka mafuta huduma yake kwa kiwango ambacho ndani ya miaka
michache jina lake lilijulikana katika maeneo ya vijijini zaidi. Popote
unapoenda katika ulimwengu huu utapata kwamba jina la Mtume huyu limekutangulia.
“(-Introduction of Morris Cerullo’s Book, Wind Over the 20th
Century)
DAVID EDWIN HARRELL JR. – “Wengi wa washiriki wa
uponyaji ulioibuka mwaka 1947 walimtazama Branham kama mwanzilishi wake.
William Branham akawa nabii kwa kizazi kizima. Usiku baada ya usiku, mbele ya
maelfu ya waamini walioogopa, aligundua magonjwa ya wagonjwa na kuwatangazia
kuponywa. Nguvu ya huduma ya Branham inabaki hadithi isiyolinganishwa katika
historia ya Harakati ya Charismatic.” (-All Things Are Possible)
DAVID EDWIN HARRELL JR. – “Wengi wa washiriki wa
uamsho wa uponyaji ambao ulianza mwaka 1947 walimtazama Branham kama
mwanzilishi wake. William Branham akawa nabii kwa kizazi. Usiku baada ya usiku,
mbele ya maelfu ya waumini waliojawa na mshangao, alitambua magonjwa ya
wagonjwa na kuwatangazia uponyaji. Nguvu ya huduma ya Branham bado ni hadithi
isiyoweza kulinganishwa katika historia ya harakati ndani ya baadhi ya makanisa
ya Kikristo ambayo yanasisitiza karama zinazoaminika kutolewa na Roho
Mtakatifu, kama vile kunena kwa lugha na uponyaji wa wagonjwa.. “ (- All things
are possible)
THOMAS R. NICKEL – “Katika siku za Biblia,
kulikuwa na Watu wa Mungu ambao walikuwa manabii na waonaji. Lakini katika
rekodi zote za kitakatifu, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa na huduma kubwa
kuliko ile ya William Branham, Nabii na Muonaji wa Mungu, ambaye picha yake
inaonekana kwenye ukurasa wa mbele wa jarida hili la Full Gospel Men’s Voice.
Branham ametumiwa na Mungu, kwa jina la Yesu, kuwafufua wafu.” (-Jarida la Full
Gospel Men’s Voice, Februari 1961)
JOSEPH MATTSON-BOZE – “Wakati mwingine nilikuwa
naogopa kutokana na mguso mkuu wa utakatifu uliopenya kwenye mkutano, lakini
kamwe sikushindwa kuona kazi ya Mungu ikifanya kazi kupitia mtumishi wake na
kuhisi joto la upendo lililopita kupitia huduma yake.” (-The Herald of Faith,
Februari 1966)
MAISHA YA AWALI NA UONGOFU
William Branham alizaliwa
Aprili 6, 1909 katika kibanda cha mbao huko kwenye milima ya Kentucky, akiwa mtoto wa kwanza kati
ya watoto tisa wa Charles na Ella Branham. Akiwa amelelewa karibu na
Jeffersonville, Indiana, alijua maisha ya umaskini mkubwa na na hali ugumu,
baba yake akiwa mlevi na asiye na elimu. Akiwa amezungukwa na hali hizi,
mvulana huyu mdogo alionekana kuwa “mwenye wasiwasi”, kwa sababu tangu utotoni
mwake alikuwa akizungumza juu ya “maono” na “sauti” iliyomzungumzia kutoka
kwenye upepo, ikisema, “Kamwe usinywe, wala usivute, wala usiutie unajisi mwili
wako kwa njia yoyote. Kutakuwa kuna kazi ya kufanya utakapokuwa mkubwa.”
William Branham alimjua Bwana na kujazwa na Roho Mtakatifu mwaka 1931. Tangu wakati huo, Biblia ilikuwa ndio hasa lengo katika maisha yake na Yesu Kristo alikuwa kitovu cha kuwepo kwake! Aliwekwa wakfu kwa ajili ya huduma akiwa na umri wa miaka 23, katika kanisa la Kibatisti mnamo Desemba ya 1932.
KUJILIWA NA MALAIKA
Tarehe 11 Juni 1933, William
Branham alikuwa akibatiza katika Mto Ohio karibu na Jeffersonville, Indiana,
mwanga mkali wa moto ulitokea ghafla juu ya kichwa chake na sauti ikasema,
"Kama Yohana Mbatizaji alivyotumwa kuutangulia ujio wa kwanza wa Yesu
Kristo, vivyo hivyo wewe umetumwa kuutangulia ujio wake wa pili!" Gazeti
la “The evening news” la Jeffersonville liliripoti tukio hilo na kuandika kichwa
kidogo cha habari, "Nyota Isiyoeleweka Yazuka Juu ya Mhubiri Wakati wa
Kubbatiza."
Mnamo Mei ya 1946, alijiweka
kando kumtafuta Mungu ili kutaka kujua hasa sababu za ya maisha yake ya ajabu.
Alipokuwa akiomba peke yake usiku mmoja, malaika wa nuru alionekana, akisema,
“Usiogope. Nimetumwa kutoka kwenye uwepo wa Mungu Mwenye Nguvu kukujulisha
kwamba kuzaliwa kwako kipekee na maisha yasiyoeleweka imekuwa ni ishara kwamba wewe
unapaswa kuleta cha uponyaji wa kiungu kwa watu duniani. Ikiwa utakuwa
mwaminifu unapomwomba Mungu na kuwafanya watu wakuamini, hakuna kitu
kitakachosimama mbele ya maombi yako, hata kansa. Utazunguka sehemu nyingi
duniani na kuwaombea wafalme na watawala na wenye nguvu. Utahubiri mbele ya
umati mkubwa kote duniani na maelfu watakujia kwa ushauri.”
Kwa nusu saa, malaika huyu
alimwelezea Ndugu Branham kuhusu mambo ya wakati uliokwishapita na kumwambia
kuhusu mustakabali wake. Alieleza kwa nini wahubiri hawakuweza kutambua karama
ya Mungu maishani mwa William, lakini shetani alikuwa na uwezo wa kutambua.
Hali ilikuwa kama ile ya siku za Yesu: viongozi wa kidini walisema Yesu ana
pepo, lakini mapepo huko Gadara walimtambua (Marko 3:22; Yohana 7:20).
ISHARA MBILI ZILIZODHIHIRISHWA
Malaika pia alimwambia Ndugu
Branham kwamba, kama vile Musa alivyopewa ishara mbili kuthibitisha alitumwa na
Mungu (Kutoka 4:1-8), vivyo hivyo angepewa ishara mbili. Kwanza, angekuwa na
uwezo wa kutambua magonjwa kwa njia ya mitetemo yake, ambayo ingesababisha
mkono wake kuvimba. Ikiwa uvimbe ungepungua baada ya kumuombea mtu, angeweza
kusema, "Hivi asema Bwana, umeponywa." Malaika alisema wakati
ungefika ambapo Ndugu Branham angeweza kutambua siri za mioyo ya watu
(Waebrania 4:12; Yohana 2:24-25).
Mamilioni ya watu
wanashuhudia kwamba maneno ya malaika yalitimizwa kikamilifu (kama ilivyo
katika Matendo 27:21-25). Ishara iliyokuwa mikononi mwake ilidhihirika, na
ilipotazamwa ingeinua imani ya watu ya kuponywa, huduma yake ilikua kitaifa,
kisha kimataifa. Kisha ikafika mahali ambapo Roho wa Kristo angefunua kwake
mawazo halisi ya mioyo ya watu, kufichua mahitaji yao, kufunua dhambi zisizotubiwa
ambazo hazikuoshwa na Damu ya Yesu Kristo; kufunua mambo kuhusu maisha yao
ambayo Ndugu Branham mwenyewe hangeweza kujua. Si kusoma akili wala saikolojia,
bali badala yake angeona maono juu ya hayo – mambo yaliyotendeka mbele ya macho
yake wazi (Yoeli 2:28). Na alipozungumza chini ya upako, katikati ya mamia mara
maelfu ya watu ulimwenguni kote, maneno aliyoyasema kwa wageni hayakushidwa kamwe
kuwa kweli kamilifu. Na unabii – wa uponyaji, wa matukio ya baadaye, madogo
hadi makubwa, mara elfu na mara elfu na mara elfu – hata mara moja hakukuwa na
kosa hata kidogo! Ilikuwa ni halisi, “HIVI ASEMA BWANA!”
Katika miaka kumi iliyofuata,
Ndugu Branham alizunguka dunia mara saba, akifanya mikutano mikubwa zaidi
katika historia. Watu takriban 100,000 walimsikia huko Durban, Afrika Kusini.
Malori saba yalichukua magongo, viti vya magurudumu, fimbo, n.k., baada ya
huduma za uponyaji.
Watu wengi wenye ushawishi kwenye
umma, ikiwa ni pamoja na Mbunge Upshaw wa Marekani na Mfalme George VI wa
Uingereza, waliponywa kutokana na sala zake.
HUDUMA ULIMWENGUNI KOTE
Habari za miujiza na uponyaji
zilipoenea, wachungaji kutoka sehemu zote walianza kumwita Ndugu William
Branham awahudumie kwenye makusanyiko yao na kuwaombea wagonjwa. Alikuwa
amepewa Ishara ya kimiujiza kwa lengo la kuwatia moyo watu wamwamini.
Kwanza, ishara ya kimwili
kwenye mkono wake ingeonyesha ugonjwa au uponyaji. Baadaye katika huduma yake,
mawazo na mahitaji ya siri za watu binafsi yalifunuliwa, na hivyo kupelekea
imani ya uponyaji. Ilikuwa wazi kwa msomaji yeyote wa Biblia kwamba William
Branham alikuwa ametiwa mafuta kuwa nabii kutekeleza unabii wa Maandiko mengi
kuhusu wakati wetu. Makanisa hayakuweza kumudu umati wa watu, na mikutano
ilihamia kwenye majengo makubwa au viwanja vya michezo kwa kampeni za pamoja
katika miji mikubwa ya Amerika Kaskazini.
Wakati akihubiri Injili ya
Yesu Kristo huko Portland, Oregon, mwanaume mwenye pepo alikwea jukwaani,
akimuita Ndugu Branham mwongo, bandia, mwendawazimu, akitishia kuvunja kila
mfupa mwilini mwake. Mtu huyo alipokaribia kutekeleza vitisho vyake, Ndugu Branham
alisema kwa upole, “Shetani, kwa sababu umemkataa mtumishi wa Mungu – kwa Jina
la Yesu Kristo, utaanguka miguuni mwangu.” Mwanaume mwenye nguvu alijaribu
kukaribia zaidi, lakini hakuweza. Alianguka chini na ilibidi abebwe na waangalizi
wa ibada kwa sababu aliangukia uso mbele ya mtumishi wa Mungu aliyethibitishwa
na Mungu.
Huko Bombay, India, ambapo
watu takribani 400,000 walikuja kusikia Injili, kulikuwa na kipofu ombaomba
aliyekuja mbele ya Ndugu Branham ili aweze kuombewa. Katika maono, Ndugu
Branham aliona kuwa huyu omba omba alikuwa nani, alikuwa anakaa wapi, na kwamba
alikuwa kipofu kwa sababu ya kutazama jua, ambalo aliliabudu kama Mungu wake. Kisha
Ndugu Branham aliwakaribisha makuhani mbalimbali wa Kihindu kwa zamu akisema,
“Ikiwa mungu wenu ni Mungu, basi njoo hapa jukwaani na mmwambie afungue macho
ya mtu huyu, na akiweza tutaona na kumsujudia huyo mungu wenu.” Hakuna thubutu
kusogea. “Lakini ikiwa Mungu wangu, Bwana Yesu Kristo, ni Mungu na atafungua
macho ya mtu huyu, je, mtaiacha miungu yenu isiyokuwa na nguvu na kumkubali
Yesu kama Mwokozi wenu?” Walikubaliana na hilo. Sababu ya kujiamini kwa Nabii
huyu ilikuwa kwa sababu alikuwa ameshaona uponyaji wa huyu mtu kwenye ono, na
maono haya kamwe hayakumwacha. Wakati macho ya mwombaji yalipofunguka na kuona
watu wote katika mkutano huo, ghasia ziliibuka huku watu maskini wakijitahidi
kumgusa Ndugu Branham ili kuponywa.
Ilikuwa huko Mexico ambapo
imani ya mwanamke ilisababisha Mungu kufanya muujiza mkubwa. Daktari aliandika
taarifa ya kiapo kwamba mtoto wake alikufa saa 9:00 asubuhi kutokana na nimonia,
lakini kwa sababu alikuwa amemwona Mungu akimrudishia mwanaume kipofu uwezo wa
kuona katika mikutano ya Ndugu Branham usiku uliotangulia, aliendelea kubeba
mtoto wake aliye kufa mchana kutwa, akiamini kwamba angefanikiwa kumfikisha kwa
Ndugu Branham, Mungu angefufua. Usiku huo, ambapo Ndugu Branham alikuwa na
mkutano, aliona maono ya mtoto wa Kimeksiko akibebwa na mama yake, akiwa hai.
Hapo aliomba kwa jina la Yesu na kuweka mikono juu ya mtoto. Mara moja mtoto
huyo alianza kulia kwa kuwa alikuwa amerejeahewa tena uhai. Habari hiyo iliandikwa
kwenye makala na daktari aliyetoa cheti cha kifo hakuweza kuamini kilichotokea.
NGUZO YA MOTO
Picha ambayo upande wake wa
kushoto kuna NGUZO YA MOTO juu ya kichwa cha Ndugu Branham ilichukuliwa huko
Houston, Texas, mwezi wa Januari mwaka 1950. Nuru hii ilikuwa ikiambatana na
Ndugu Branham tangu kuzaliwa kwake mwaka 1909. Na wakati wa huduma ya ubatizo
mwaka 1933 katika Mto Ohio huko Jeffersonville, Indiana, KIUMBE HIKI CHA KIMBINGUNI
kilitokea mbele ya mamia ya watu kikimwambia, “Kama Yohana mbatizaji
alivyotangulia kuja kwa Kristo mara ya kwanza, wewe utatangulia kuja kwake mara
ya pili.” Picha hii inaoneshwa leo katika Maktaba ya Congress huko Washington,
D.C. na ilifanyiwa uchunguzi na kuthibitishwa kuwa halisi na Bwana George Lacy,
mtathmini wa Nyaraka zenye viulizo/mashaka nchini Marekani, kuwa hati pekee ya
kweli ya nguvu za kiungu katika kizazi hiki.
WINGU LA AJABU
Mnamo Februari 28, 1963, huko
Arizona, Marekani, kundi nyota la malaika saba lilimtokea Mchungaji William
Marrion Branham kwa mfumo wa wingu lenye umbo la pete.
Hawa malaika saba walitoka
mbele za Mungu wakimfunulia siri zilizofichwa za Biblia zilizokuwa zimetiwa
mhuri katika Kitabu cha Danieli na Kitabu cha Ufunuo, ingawa zilikuwa zimewekwa
wakfu kufunuliwa wakati wa mwisho. Hii ilikuwa kwa lengo la kuwajulisha watu wa
Mungu kuhusu mapenzi kamili ya Baba katika maandalizi ya utawala wa milenia wa
Yesu Kristo juu ya dunia hii.
Ilivyokuwa walipoondoka machoni
pa Ndugu Branham ndipo walipounda hili wingu la ajabu ambalo lilichapishwa kwenye
Jarida la Life toleo lao la Mei 17, 1963, na Jarida la Sayansi katika toleo lao
la Aprili 19, 1963.
Picha asilia zenye mwangaza
zinaonyesha uso kamili wa Bwana Yesu Kristo huku picha ikionekana kutoka
pembeni kulia “kama Mwana wa Adamu, kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe
kama sufu, nyeupe kama theluji” (Ufu. 1:13).
Vitabu saba vya ufunuo
vilivyotiwa muhuri vilifunuliwa
Mnamo Desemba 22, 1962, Ndugu
Branham aliona ono alipokuwa amesimama karibu na Tucson, Arizona, alikuwa akitoa
mchanga kwenye suruali yake, wakati mlipuko mkubwa ulitokea. Alieleza ono hili
kwa waumini wake huko Jeffersonville, Indiana mnamo tarehe 31 Desemba (mahubiri
yalirekodiwa kwenye kanda). Baadaye akahamia Tucson, Arizona.
Zaidi ya mwezi mmoja baadaye,
tarehe 28 Februari, 1963, alipokuwa akienda kuwindwa, aliona mchanga kwenye
suruali yake. Alipoinua mkono kuitoa, mlipuko mkubwa ulitikisa upande wa mlima.
Akiangalia juu, aliona malaika saba wakija kwake kwa mfumo wa piramidi, na kwa
muda alionekana kusimama katikati yao. Hawa malaika saba wanawakilisha Wajumbe
Saba wa Nyakati Saba za Kanisa kama ilivyoandikwa katika Ufunuo sura ya 2 na 3.
Kisha sauti ikapaza, “Rudi
upande wa mashariki,” na Ndugu Branham alijua ilikuwa wakati wa kufunuliwa kwa
siri za Mihuri Saba katika Kitabu cha Ufunuo (Danieli 12:4,8-9; Ufu. 5,6 na 8)
ambazo malaika walimkabidhi. Malaika walirudi angani na kuunda wingu lenye
urefu wa maili 50 na upana wa maili 30, ambalo lilikuwa linaweza kuonekana kwa
mamia ya maili mbali.
Picha nyingi za Wingu hili la
kipekee zilichukuliwa, baadhi zilichapishwa katika Jarida la Life (toleo la Mei
17, 1963); nyingine katika Jarida la Sayansi (toleo la Aprili 19, 1963), pamoja
na ripoti ya kisayansi jinsi ilivyokuwa haiwezekani kisayansi kwa wingu kama
hilo kuwepo. Wingu la juu zaidi hujitokeza takribani maili 10, lakini wingu
hili la kushangaza lilikuwa maili 26 juu, ambapo unyevunyevu wa maji hauwepo.
Ndugu Branham alirudi
Jeffersonville, Indiana ambapo kwa siku saba, akimngojea Mungu, sauti ya Mungu
iliongea kupitia Nguzo ya Moto, ikifunua Ukweli kamili wa Siri zilizofungwa
katika Ufunuo 5 hadi 8; ufunuo ambao ulikuwa kinyume na ule ambayo kila mtu
(ikiwa ni pamoja na Ndugu Branham) alikuwa amefikiria awali, lakini ulikuwa
kamili kulingana na Neno lote la Mungu.
Kama Ndugu Branham alihubiri siku
saba mfululizo kuhusu hizi Mihuri (Machi 17-24, 1963), mahubiri yake
yalirekodiwa kwenye sauti: Hivyo Maandiko yanatimia katika siku zetu yakisema,
“Lakini isipokuwa katika siku za sauti ya malaika wa saba atakapokuwa tayari
kupiga baragumu; hapo ndipo siri ya Mungu itakapotimizwa, kama alivyowahubiri
watumishi wake hao manabii.” (Ufu. 10:7).
MAONO SABA YA WILLIAM BRANHAM
Katika mwaka wa 1933, Mungu
alimpa Ndugu Branham maono mwendelezo ya mambo saba makuu ambayo lazima yatokee
kabla ya Bwana Yesu Kristo kuja tena.
Ono la kwanza
(1) ilikuwa kwamba aliona dikteta akiinuka nchini Italia ambaye angeivamia
Ethiopia. Alimwona Mussolini na mwisho
wake wa aibu ambapo watu walimgeukia, kabla haijatokea katika tukio halisi.
Ono la pili
(2) alionyeshwa na Mungu ambapo alimwona kijana Mwaustria aliyeitwa Adolf
Hitler ambaye angepata mamlaka/nguvu nchini Ujerumani na angeuibgiza ulimwengu
kwenye vita, na kwamba Ujerumani ingeshindwa na Hitler angefikia mwisho wa kutatanisha.
Katika ono la tatu (3),
aliona ITIKADI tatu kuu ulimwenguni: Ufashisti, Unazi na Ukomunisti: lakini
zile mbili za kwanza zingemezwa na ile ya tatu – Ukomunisti.
Kisha katika ono la nne (4),
aliona maendeleo makubwa sana ya sayansi ambayo yangefuatia baada ya vita vya
Pili vya Dunia. Aliona gari likionekana
kama yai ambalo linaendeshwa si na wanadamu bali kwa udhibiti wa mbali (Rimoti).
On la tano
(5) alioneshwa upotovu wa kutisha wa kimaadili duniani, hasa kwa
wanawake. Aliwaona wanawake wakikata
nywele zao, wakivuta sigara, wakinywa pombe, wamevaa suruali na mavazi
yasiyofaa. (Kumbuka mambo haya matano
alionyeshwa mwaka 1933, miaka kadhaa kabla hayajatokea).
Katika ono la sita (6),
aliona mwanamke mrembo, lakini mkatili akiinuka Marekani, akitawala nchi kwa
mamlaka.
Na katika ono la mwisho
(7), aliona nchi ya Marekani katika magofu yanayofuka moshi. Kwa kadiri macho yalivyoweza kuona hapakuwa
na uhai, ila mashimo tu na marundo yanayofuka moshi. Pia aliona Los Angeles, California ikizama
chini ya bahari kutokana na tetemeko kubwa la ardhi. Kisha maono haya yakapotea.
UNABII ULIOTIMIA KATIKA SIKU
ZETU
“Hakika Bwana MUNGU hatafanya
neno lo lote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.” Amosi 3:7
Mpango wa Mungu wa
kushughulika na watu wake daima umehusisha kutuma manabii. Nabii Amosi
anatuambia kwamba Mungu hafanyi “jambo lolote” bila kuwa na mtangulizi nabii,
na hata utafiti wa haraka wa historia ya Maandiko utathibitisha hili kuwa
sahihi. Ni mara chache ambapo alitokea nabii kuhubiri neno la Mungu ambaye
hakukutana na kutiliwa mashaka, kukataliwa na kutukanwa!
FIKIRIA Maandiko haya juu ya
roho ya Eliya:
MALAKI 4:4-6 “Angalieni,
nitawapelekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya BWANA, iliyo kuu na
kuogofya. Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto
iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana.”
Malaki 4:5 na 6 ina sehemu mbili, imetimizwa
kwa sehemu katika huduma ya Yohana, Mbatizaji. Alitangulia ujio wa kwanza wa Yesu Kristo,
unaoitwa siku “kuu” ya Bwana, akigeuza mioyo ya baba wa “torati” kuelekea
watoto wa enzi ya “neema” ya Agano Jipya.
Kama ilivyoelezwa katika
Maoni ya Biblia nzima ya Jamieson, Fausset & Brown, “…Yohana mbatizaji alikuwa
Eliya katika roho (Luka 1:16,17) lakini si Eliya halisi (Yohana 1:21). Hii ina
maana kwamba Yohana, akijua kwamba alitajwa na Malaki 4:5, alijua kwa ufunuo
kwamba hakuweza kutekeleza kikamilifu yote yaliyomo katika unabii huo: kwamba
kuna kutimiliza zaidi. Kuna nabii atakayetimiza sehemu ya pili ya maandiko
haya, akiandaa njia kwa kuja kwa pili kwa Kristo na “kugeuza mioyo ya watoto kuwaelekea
baba zao…” Kwa maana halisi, hii inamaanisha kutakuwa na huduma itakayogeza
mioyo ya kizazi kilichopotea kurudi kwenye Neno la Mungu na imani ya baba wa
“kanisa la mwanzo” kabla ya “siku ya kutisha ya Bwana”, kuja kwa pili kwa
Kristo kwa hukumu.
Tena, Mathayo
17:10-12 ina sehemu mbili.
Kwanza, “Mbona basi waandishi hunena ya kwamba imempasa Eliya kuja
kwanza?” “… Lakini nawaambia,
ya kwamba Eliya amekwisha kuja wala hawakumtambua…” akizungumzia Yohana
Mbatizaji. Pili, “Na Yesu akajibu,
akawaambia, Eliya atakuja kwanza, na kutayarisha mambo yote.” Akizungumza juu ya mtangulizi wa wakati ujao
wa kutangulia kuja kwa pili kwa Kristo.
Huduma ya William Branham ni
utimilifu wa ujio wa roho wa Eliya ambao ungetangulia ujio wa pili wa Kristo
ambao ni “kurejesha” mioyo ya watoto kwenye mafundisho ya Mababa Mitume.
Huduma ya William
Branham ilihusisha hatua tatu tofauti ambazo alizitaja kama “mivuto”. Mvuto wa Kwanza: Uponyaji. Mvuto wa Pili: Kutabiri/unabii. Mvuto wa Tatu: Kufungua au kufunua Neno la
Mungu.
Huduma ya Yesu
Kristo ilifuata mtindo uleule. Mvuto wa
Kwanza: makundi ya watu yalimiminika ili kusikia maneno yake ya neema na
kupokea mguso Wake wa uponyaji wa kimiujiza.
Mvuto wa Pili: Alitambua siri za mioyo. (Yohana 4:17-18) Mvuto wa Tatu: “Ujumbe”
wake, Neno la Mungu lililokuja kwa nguvu kinyume na utaratibu wa kidini wa siku
hiyo, na kusababisha umati kumwacha.
“Tangu wakati huo wengi wa wanafunzi wake walirudi nyuma, wasiandamane
naye tena.” Yohana. 6:66
WAJUMBE WA MUNGU WA WAKATI WA
MWISHO
NABII HAKOSI HESHIMA ISIPOKUWA
KATIKA NCHI YAKE MWENYEWE.
Kwa nini basi William Branham
hafahamiki sana leo?
Hakuna Nabii wa kweli aliyewahi kukubalika na wengi katika wakati wake. Lakini
nabii wa kweli anapinga uovu wa wakati wake, na watu hawapendi kubadilika
kutoka njia zao za kimwili. Ni wachache tu watakaofahamu na kuamini, kama
ilivyokuwa siku za Yohana Mbatizaji.
Angalia hili: maadamu Yesu
Kristo (ambaye alikuwa ni Nabii-Mungu) alipokuwa akiwaponya wagonjwa, umati wa
watu ulimsonga. Lakini alipoanza kutoa mafundisho
yenye nguvu, akiwakemea Masadukayo na Mafarisayo (madhehebu ya siku zake),
Biblia inasema hivi: “Tangu wakati huo wengi wa wanafunzi wake walirudi nyuma,
wasiandamane naye tena,” (Yohana 6:48-68).
Vivyo hivyo, mradi Mungu
alimtumia Ndugu Branham kuponya wagonjwa na wanaoteseka, mamilioni walifuata
huduma yake. Lakini Mungu kupitia nabii
wake alipoanza kurejesha NENO, watu wengi walipenda miujiza lakini walichukia
Neno. Hata hivyo, Neno lilipaswa
kurejeshwa kabla Yesu Kristo hajamchukua Bibi-arusi Wake, kwa maana hana budi
kuwa Bibi-arusi wa Neno safi, na maana ya kweli la Neno la Mungu imepotoshwa
sana kote katika karne zote mpaka leo;
kama Yesu alivyosema, “Nao waniabudu bure, wakifundisha mafundisho
yaliyo maagizo ya wanadamu … wakilitangua Neno la Mungu kwa mapokeo yenu”
(Marko 7:6,7,13).
Msidhani ya kuwa mambo hayo
humwinua mtu, KRISTO PEKE YAKE AMEINULIWA!
Ndugu Branham mwenyewe hangeweza kufanya lolote (Yohana 3:27). Ilikuwa ni Yesu Kristo akifanya (kupitia nabii
mnyenyekevu) kazi zile zile alizofanya alipotembea katika mwili wa mwanadamu
hapa duniani (Ebr. 13:8). Kwa hiyo
usimtazame mtu huyo, bali tazameni Ujumbe aliouleta, kwa maana Ujumbe huo
utakuelekeza kwa Yesu Kristo aliye safi, ambaye hafungamani na kanuni na
mapokeo yote ya kimadhehebu.
Je, mtume Paulo hakusema, “Iweni
wafuasi wangu, kama mimi nilivyo mfuasi wa Kristo,” (1Kor. 11:1; 4:16). Unapomtii Paulo, humfuati mtu, bali Roho
Mtakatifu anayesema kupitia kwake. “Na
leo,” kama mtu mmoja alivyoandika, “mtu huyu, William Branham, amekuwa na
maelfu ya uthibitisho uliodhihirishwa kutoka kwa Mungu, na maisha yake yakiwa
na mambo mengine yote yanayounda ofisi ya unabii, anapaswa kupokelewa – lazima
apokelewe kwa jinsi alivyo. “Bwana asema
hivi” katika kinywa chake kwa Roho Mtakatifu, si tofauti kabisa na “Bwana asema
hivi” katika kinywa cha Paulo, kwa maana ni Roho Mtakatifu yeye yule.
Lakini je, ungemtambua Paulo
kama ungaliishi katika siku zake? Au
kama uliishi siku za Nuhu? Au
Eliya? Au Yeremia? Je! Ungewatambua kama manabii na kutii Ujumbe
wao? Vipi kama ungeishi sehemu ya mbali
ya Palestina na kusikia taarifa kuhusu mtu anayeitwa Yesu ambaye alikuwa
akifanya miujiza mikubwa? Je!
Ungemtambua kuwa Yeye ni nani, au ungekuwa kama Mafarisayo, ambao waliamini
yale ambayo Mungu alifanya zamani, lakini hawakuweza kukubali kile ambacho
Mungu alikuwa akifanya katika siku zao wenyewe!
Hata walimwita Yesu “Beelzebuli, mkuu wa mapepo”. “Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki!
Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki, na
kusema, Kama sisi tungalikuwako zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao
katika damu ya manabii. Hivi mwajishuhudia wenyewe, ya kwamba ninyi ni wana wao
waliowaua manabii.”( Mt. 23:29-31 ).
UJUMBE WA MWISHO ULIOACHWA
KWA SISI WOTE.
William Branham alikufa mnamo
Desemba 1965 wakati gari lake lilipogongwa na dereva mlevi. Kilikuwa ni kifo ambacho tayari alikitarajia
kwa maono. Lakini UJUMBE ambao Mungu
alimtumia kuleta uhai hauwezi kufa. Hivi
leo kuna zaidi ya mahubiri 1,100 tofauti ya Ndugu BRANHAM yaliyorekodiwa kwenye
kanda na mengi ya haya yamechapishwa katika mfumo wa vitabu vinavyozunguka
dunia nzima, yakilia dhidi ya upotovu, yakiwaonya watu kwamba Yesu Kristo
anakuja upesi sana, yakifunua ukweli kupitia Neno la Mungu, na kumwandaa
Bibi-arusi kwa ajili ya Kuja kwa Pili kwa Yesu Kristo. Ni “sauti ya mjumbe wa saba” na Ujumbe wa
Neno wa mwisho kwa wakati wetu.
Mungu kwa mara nyingine tena
ametembelea kizazi hiki cha mwisho kupitia nabii mkuu. Mtu mnyenyekevu, ambaye hakutamani umaarufu
wala mali, ambaye hakukosa kamwe kutoa kila sehemu ya utukufu kwa Bwana Yesu
Kristo.
Kwa kifupi makala hii imeonesha
maisha yake, kwa ufupi na uthibitisho wake.
Hata hivyo, hii haijagusa hata Ujumbe alioleta, ingawa ni Ujumbe huo ndio
muhimu zaidi. Sasa ni juu yako kuchimba zaidi
hazina hizi. Vitabu na kanda
zinapatikana endapo utahitaji, lakini lazima uwe mwaminifu kuchunguza, kupima
uthibitisho, kulichunguza Neno, na kisha kuomba. Kama ni Kweli, Mungu anakuhitaji uiamini.
Hatimaye Ndugu Branham
alihitimisha: “Tuko mwishoni, marafiki.
Hivi karibuni wakati utaisha.
Mamilioni watapoteza maisha.
Mamilioni ambao sasa wanaamini kuwa wameokolewa watahesabiwa kuwa chakula
wakati huu wa atomiki. Tunaishi katika
saa ya mwisho. Kwa neema ya Mungu, kwa msaada
wake tunazungumza na watu wake ili wapate kutazamia kuja kwake Kristo upesi…”
Tufuate kwenye Mitandao