UTANGULIZI.

KRISMASI ilitokana na neno "Misa ya Kristo" ambayo ni desturi ya Wakatoliki wa Roma, misa maalum inayofanywa kusherehekea kuzaliwa kwa Kristo.

Krismasi haikuwa miongoni mwa sherehe za awali za Kanisa la Kikristo. Haikuadhimishwa, kutolewa heshima, wala kufuatiliwa, na mitume wala katika kanisa la mitume, kwa miaka 300 ya kwanza ya historia ya kanisa, baada ya Ukatoriki kuchukua uongozi wa kanisa la kwanza la Rumi lililokuwa limeanzishwa awali na Mtume Paulo. Ilikuwa mwaka 350 A.D. ambapo Papa Julius-I alitangaza kwamba kuzaliwa kwa Kristo kunapaswa kuadhimishwa "Desemba 25". Historia inaonyesha kuwa Kanisa huko Yerusalemu lilianza kuadhimisha Krismasi tu mwaka 440 A.D., kufuatia shurutisho la Ukataliki wa Kirumi.

HISTORIA YA KALE

Historia ya zamani inaonyesha kwamba katika tamaduni za kale za kipagani, sio jambo la bahati mbaya kwamba Desemba 25 pia ilikuwa siku ya kuzaliwa kwa miungu yao ya kipagani. Sherehe zote za KIBABELI na za KIRUMI ziliambatana na kipindi cha sherehe cha muda wa siku 5-7 cha shangwe isiyo na kizuizi au ulevi na uasherati kati ya tarehe 17 na 23 Disemba. Desemba ni wakati wa mwaka ambapo mchana huanza kurefuka na mwanadamu wa zamani alibarikiwa na “ujenzi upya wa asili” na kufanya sherehe ya kila mwaka kwa ajili yake.

Tarehe 25 Desemba ilikuwa Sherehe ya Ushindi wa “Mungu Jua” katika ulimwengu wa Kibabiloni ya kipagani. Katika Dola la Rumi la zamani, sherehe sawa na hizo zinaweza kufuatiliwa kwenye Sherehe ya Kirumi iliyoitwa “Saturnalia,” iliyoadhimishwa kwa lengo la kutoa heshima kwa Saturn, mungu wa mavuno, na Mithras, mungu wa mwanga. Walifanya sherehe ya sarakasi kipindi hiki cha mwaka. Sherehe zote mbili zilisherehekewa wakati wa solstice (wakati jua linaonekana upande wa kaskazini kwa dunia wakati wa majira ya baridi) ya majira ya baridi, kati ya tarehe 17 na 23 Disemba.

 “MJUMBE WA MWISHO ANASEMA NINI KUHUSU “KRISMASI””?

Kwa wale wanaoamini katika Ujumbe wa Mwisho wa Wakati huu, sote tunatambua kwamba Mungu alitutumia nabii aliyethibitishwa kwa ajili ya kipindi hiki ili kurudisha mioyo yetu kwenye IMANI ya Wazee wa Pentekoste na kufundisha kweli ya Biblia. Wakati huo huo, alitumwa na Mungu kutufunulia MISTARI YOTE iliyojificha katika Neno, kulingana na agizo la unabii alilopewa kama ilivyoonyeshwa katika Malaki 4:5-6 na Ufunuo 10:7. Kwa hiyo, kutoka mtazamo huu, nataka kuelezea suala hili lenye utata kuhusu “Krismasi”.

Ufuatao ni muhtasari wa maelezo muhimu kutoka kwenye mahubiri ya Ndg William Marrion Branham kuhusu kusherehekea siku ya Krismasi. Unapaswa usome katikati ya mistari.

1.     KRISTO ALITUREJEZA KWENYE KIFO CHAKE NA SIO KUZALIWA KWAKE.

Krismasi haitajwi katika Kitabu chote cha Biblia. Hakuna wakati hata mmoja Yesu aliwahi kuwarejesha kwenye kuzaliwa Kwake, bali kwenye mauti Yake.

61-1224 - Mabwana, Sisi Tunataka Kumwona Yesu

2.     YESU KRISTO HAKUZALIWA MWEZI WA DESEMBA; ALIZALIWA MWEZI WA APRILI.

Isingeweza kuwa ni siku ya kuzaliwa kwa Kristo. Kamwe isingewezekana kuwa. Angepaswa azaliwe Marchi ama Aprili, maana Yeye alikuwa ni Mwana-Kondoo. Naye alikuwa ni mwana-kondoo dume na akazaliwa chini ya kondoo dume, Kondoo. Ilibidi iwe hivyo, unaona. Na kondoo hawazaliwi Desemba hata hivyo. Kondoo huzaliwa katika majira ya Kuchipua. Na tena jambo lingine, vilima vya Yuda sasa, kuna futi ishirini za barafu juu yake. Wachungaji wangaliwezaje kuwa huko nje?

64-1227 - Mnasema Huyu Eti Kuwa Ni Nani?

Sasa, Krismasi si sherehe ya Kiprotestanti. Ni siku ya Kikatoliki. Tarehe 25 Desemba ilikuwa miezi na miezi kabla ya ninii yetu…baada ya…au kabla Bwana wetu hajazaliwa. Bwana wetu alizaliwa Aprili. Lakini hakuzaliwa Desemba. Ikiwa umekuwa katika Uyahudi, mnamo Desemba, ni baridi zaidi kuliko hii, kwa hivyo—kwa hivyo unajua Yeye hakuzaliwa Desemba. Na inaandikwa, ni K-r-i-s-m-a-s-i, misa kwa ajili ya Kristo. Ni misa ya Kristo.

54-1219M - Uponyaji Wa Kiungu
Na jambo lingine, wala Kristo hakuzaliwa tarehe ishirini na tano Desemba. Isingewezekana Kwake. Kama ulipata kuwa Uyahudi, vilima vimejaa theluji, vibaya sana kuliko ilivyo hapa. Alizaliwa Aprili wakati maumbile yote yanapochipusha.

Sasa, bali ni mapokeo yao. Na ni kwa nini—kwa nini tunafanya mambo hayo? Ni kwa sababu tunafuata mapokeo ya wanadamu badala ya amri za Mungu. Hao…Kitu kama hicho kisingejalisha, bali wanaifanya tu kuwa ni siku ya biashara. Ni fedheha, aibu kwao kufanya vitu kama hivyo.

 60-1204E - Ono La Patimo

3.     KRISMASI ILITOKANA NA SHEREHE YA MUNGU JUA WA WARUMI.

Tunasherehekea siku hii ya 25 ya Desemba kwa ajili ya siku ya kuzaliwa kwa Kristo, bali, kwa kweli, mtu yeyote anajua ya kwamba haikuwa siku ya kuzaliwa kwa Kristo. Hiyo ilikuwa ni siku ya kuzaliwa kwa mungu-jua wa Rumi, ambapo kanisa lilipobadilishwa kuingia, au, kuingizwa katika Ukatoliki, iliundwa kwenye baraza huko Nikea. Badala ya hiyo kuwa ya “mungu-jua,” waliifanya siku ya kuzaliwa kwa “Mwana wa Mungu.” Huo ulikuwa ni wakati, jua, ni kuanzia tarehe 20 mpaka…ninamaanisha tarehe 21 hadi 25, kwa namna fulani liko kwenye ninii yake…Nasahau ni jina gani mnaiita, hasa. Ni wakati labda ni mara mbili au mara ya pili linapopita katika hatua hiyo. Na ilikuwa ni siku ya kuzaliwa kwa mungu-jua, nao wakachukua tu “Mwana wa Mungu” na kufanya hiyo siku ya kuzaliwa Kwake, kuioanisha na desturi yao ya kikafiri. Na hakuna njia, hata kidogo, hiyo kuwa siku ya kuzaliwa kwa Kristo.

Asingeweza kuzaliwa wakati huo, kwa sababu Uyahudi uko karibu sawa kwenye—kwenye ninii…juu kwenye ikweta, kama hii ilivyo, na sisi—sisi tunaona kwamba, katika Uyahudi, wakati wa baridi kali, tarehe 25 Desemba, una dhoruba kali ya theluji na baridi. Wachungaji hawawezi kuwa juu ya kilima, na sababu nyingi isingeweza kuwa.

Halafu basi Yeye alizaliwa kimaumbile, kama vile maumbile mengine yote, Yeye—Yeye alikuja katika majira ya Kuchipua. Kwa kawaida wakati wana-kondoo wanapozaliwa, majira ya Kuchipua; na Yeye alikuwa ni Mwana-kondoo. Sasa, ninaamini, Yeye alizaliwa, mimi mwenyewe, Machi, Aprili, ama mahali fulani karibu hapo, mwanzoni mwa majira ya Kuchipua.

63-1127 -  Ulimwengu Unaporomoka Tena

Lakini, hii ikiwa ni tarehe 25 Desemba, mbona, wakaifanya siku ya kuzaliwa, hii ni siku ya kuzaliwa kwa mungu-jua. Mnaona? Baalimu wa Kirumi, mungu-jua. Mnaona? Nalo jua liko katikati ya mzunguko sasa. Na kuanzia tarehe 20 hadi tarehe 25 ilikuwa ndiyo wakati sarakasi za Kirumi zilikuwa zikiendelea, katika kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa mungu-jua. Na kwa hiyo wakasema, “Vema, sasa, kuwafurahisha Wakristo na wapagani pia, tutafanya, badala ya mungu-jua, Mwana wa Mungu na mungu-jua, pamoja. Kwa hiyo tutazichanganya zote pamoja na kufanya siku ile ile ya kuzaliwa, na tuifanye iwe tarehe 25.” Kwa hiyo ilionekana kuwafurahisha makafiri na kanisa la kawaida wakati huo, kwenye kanisa la kwanza la Kirumi. Ilikuwa ni ninii tu…Ilikuwa tu ni sawa kwao, kwa hiyo hawakujali. Kwa hiyo wakaifanya siku ya kuzaliwa kwa mungu-jua na ya Mwana wa Mungu.

61-1224 -Mabwana, Sisi Tunataka Kumwona Yesu

Hili lilifanywa na kanisa Katoliki la Kirumi kabla halijakuwa kanisa Katoliki huko Roma. Yapata 606 B.K., mahali fulani hapo, ama 306, hasa. Sasa, tunaona ya kwamba makafiri wa Kirumi walimwabudu Jupita, ambaye ni mungu-jua; pia walimwabudu Ashtorethi, ambaye alikuwa mungu-mwezi, ama vinginevyo mama wa…ma—mama wa mbinguni. Vema, kulielezea hili dhahiri, wao walisema ya kwamba Ashtorethi, ama mungu, mama wa mbinguni hakuwako tena, naye alijiakisi katika Mariamu. Kwa hiyo ingali ilibaki ni ibada ya sanamu, ikiunganisha Ukristo na uabudu sanamu.Halafu pia, na waliteseka, ama waliabudu na kuiheshimu siku ya kuzaliwa kwa mungu-jua wao, ambaye alikuwa ni Jupita.

Ni wakati ambapo jua kutoka tarehe moja Desemba mpaka tarehe ishirini na tano Desemba, halibadiliki, linapitia kaprikoni yake.

62-1216 -Kuporomoka Kwa Ulimwengu

Lakini basi wakati Ukristo ulipoingizwa katika Urumi na kuchanganywa kule Nikea, basi walikuwa na mungu-jua, Jupiter, mungu-jua wa Rumi, siku yake ya kuzaliwa ilikuwa kwenye…kati ya…yapata siku ya ishirini na tano ya Desemba. Kwa sababu, sarakasi ya Rumi ilianza tarehe ishirini na moja na kuendelea mpaka tarehe ishirini na tano, ambayo ilikuwa katika kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa mungu-jua. Kwa hiyo kuingiza upagani wa Kirumi katika—katika Ukristo, walisema, “Hebu tuifanye siku ya kuzaliwa kwa Mwana wa Mungu, ndipo basi tunaweza sote kukubaliana juu ya hiyo.” Unaona, daima imekuwa ni juu ya mifumo ya kupatana juu ya Kweli, kila wakati, daima imekuwa hivyo.

63-1216 -Tumeiona Nyota Yake Na Tumekuja Kumsujudia

Pergamo ilialikwa. Vema, walialikwa kwenye karamu baada ya Baraza la Nikea. Walialikwa kwenye karamu ya Solistasi ya Kipupwe; ambayo inamaanisha, “jua, kuliabudu jua,” ambalo lilikuwa ni mungu wa kipagani; ambayo ilifanyiwa mnamo Desemba 21, siku iliyo fupi kuliko zote katika mwaka. Na miaka…Wakati uo huo haubadiliki mpaka Desemba 25. Makafiri wote waliisherehekea, siku ya kuzaliwa mungu-jua. Siku ya kuzaliwa kwa mungu-jua ilikuwa ndiyo siku fupi kuliko zote katika mwaka, Desemba 21. Halafu mtu yeyote aliyepata kuisoma historia ya makanisa anajua ya kwamba makafiri huabudu kwenye siku hiyo. Ilikuwa ni sherehe.

Vema, Warumi walikuwa na…walikuwa na michezo mikubwa, sarakasi za Kirumi. Ni wangapi wameiona hii hapa, chochote ilichokuwa, hapa si muda mrefu uliopita, waliyoitoa? Ben Hur! Mnaona? Sasa, sarakasi za Kirumi; hizo ndizo Warumi walizokuwa nazo kwenye siku hiyo ya jua, katika kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa ya mungu-jua. Mnaona?

60-1207 -Wakati Wa Kanisa La Pergamo

4.     KRISMASI SI KITU ZAIDI YA KUWA JAMBO LA KIBIASHARA

Leo hii, Krismasi inamaanisha pakiti ya sigara za Camels, pakiti ya Viceroy, chupa ya Four Roses ama Seagramu, zilizofungwa kwenye karatasi nzuri ya Baba Krismasi.

60-1225 -Zawadi Ya Mungu Iliyofungwa

Lakini imefikia mahali ambapo ni—ni—ni laana kwa watoto wadogo. Maskini jirani fulani huko chini mtaani anaweza kuwa na mengi, na maskini jamaa huyo mwingine hana kitu, nao wanaangalia. Na ni—ni kwamba kitu hicho chote ni kosa. Hivyo tu.

62-1216 -Kuporomoka Kwa Ulimwengu

Na yote ni hadithi za uongo tu, wala Kristo hayumo ndani yake hata kidogo. Na watu wamegeukia kwenye kununua wiski, na—na kucheza kamari, na mitindo. Na m—mtu ambaye…mfanyabiashara ambaye anaweza kuuza bidhaa zake msimu wote wa Krismasi anaweza kuishi mwaka mzima, karibu mwaka mzima uliosalia. Unaona? Ni likizo kubwa sana, kibiashara. Na maskini watoto wadogo mtaani; ambao wazazi wao hawawezi ku—kuwatembelea na za—zawadi, kama ile inayotoka kwa Baba Krismasi, basi wanatembea mtaani, huku maskini mikono yao ni michafu na macho yao ni mekundu. Na—nachukia kabisa kuiona ikija. Inapaswa kuwa ni siku yenye uchaji ya kumwabudu Mungu, badala ya kuugua moyo na kuumwa na kichwa na hayo mambo yanayotendeka. Hakuna kitu kwa Kristo juu ya jambo hilo. Lakini tuko katikati ya haya yote sasa.

64-1227 -Mnasema Huyu Eti Kuwa Ni Nani?

Katika majuma machache, ama hata sasa hivi, kuna kulungu na akina Baba Krismasi na—na milio ya kengele na kila namna ya vitu vikining’inizwa, ambayo ni sherehe ya kipagani. Ni kanuni ya kanisa Katoliki. Watu wakilipa gharama kubwa na kubadilishana zawadi na vitu kama hivyo, upagani! Krismasi ni siku ya kuabudu.

Na jambo lingine, wala Kristo hakuzaliwa tarehe ishirini na tano Desemba. Isingewezekana Kwake. Kama ulipata kuwa Uyahudi, vilima vimejaa theluji, vibaya sana kuliko ilivyo hapa. Alizaliwa Aprili wakati maumbile yote yanapochipusha.

Sasa, bali ni mapokeo yao. Na ni kwa nini—kwa nini tunafanya mambo hayo? Ni kwa sababu tunafuata mapokeo ya wanadamu badala ya amri za Mungu. Hao…Kitu kama hicho kisingejalisha, bali wanaifanya tu kuwa ni siku ya biashara. Ni fedheha, aibu kwao kufanya vitu kama hivyo. Sherehe ya kipagani! Ni lini Baba Krismasi alipata kuwa na uhusiano wowote na Yesu? Ni lini sungura wa Pasaka ama kuku ama…waliotiwa rangi kwa namna fulani ya wino ama chochote kile, ama namna fulani ya sungura mdogo mweupe walipata kuwa na uhusiano gani na kufufuka kwa Yesu Kristo? Hivi hamwoni jinsi ulimwengu wa kibiashara…?

60-1204E -Ono La Patimo

Loo, ndugu, dada, jinsi ingekuwa vizuri kama kila mmoja wenu, kama kila mmoja wetu, sisi, mimi, kama kila mmoja wetu angeweka kando haya yote hapa mapambo ya Krismasi, unaona, tuachane na huku kote kubadilishana zawadi, mmoja na mwingine, upuuzi huu wote wa ulimwenguni; na kuondoa tu majivuno yetu na kuyaweka chini, na kukanyaga kitu hicho chini ya mguu, tuseme, “Bwana Yesu, niongoze hadi kwenye ile Nuru kamilifu.” Angalia jambo fulani la Kimbinguni likitendeka. Roho Mtakatifu atakuja kwa njia ya ajabu. Mnaona?

63-1216 -Tumeiona Nyota Yake Na Tumekuja Kumsujudia

Sema, “Ninataka kufuata, ninataka kuifuata Nyota ya Asubuhi, Kristo. Ninataka kufuata na kumpata Yesu wangu leo hii. Ninataka kuondokea haya yote hapa mapambo ya Krismasi na kadhalika, kwa sababu siku moja yatateketezwa na moto usiozimika.” Na wale wote wanaochukuliana nayo, watateketezwa pamoja nayo.

63-1216 -Tumeiona Nyota Yake Na Tumekuja Kumsujudia

Mbona, walianza kununua zawadi za Krismasi miezi kadhaa iliyopita, na ni kitu gani ila tabia ya kikafiri! Hakuna kitu ambacho ni cha kiungu juu ya jambo hilo. Loo, wanajaribu kusema, “Kutoa zawadi, kwa mamajusi.” Hilo ni o—oasisi tu kwa udhuru wa ibilisi. Ukitaka kutoa kitu, ni maisha yako kwa Kristo. Msipeane mmoja kwa mwingine, mpeni Yeye. Hicho ndicho Yeye alifia. Hilo ndilo kusudi Lake la kuja.

62-1216 -Kuporomoka Kwa Ulimwengu

5.     KRISMASI NI HADITHI NA SHEREHE YA WAPAGANI.

Tulichukue neno Krismasi. Ni kwa nadra sana unapata kusikia Jina la Kristo likitajwa. Hulisikii likitajwa. Taa na vivutio vyote viko kwenye Baba Krismasi, sio kwa Kristo, hata ni vigumu kwa watu kujua Krismasi kweli inahusu nini. Wameifanya tu ya kikafiri na kuifanya ya kikafiri sana, mpaka yote imekuwa ni upagani.

61-1224 -Mabwana, Sisi Tunataka Kumwona Yesu

Nikisoma juu ya hadithi za kubuni na hadithi hizi zote za uwongo, Krismasi yenyewe ni hadithi ya uwongo. Si ninii…Hakuna kitu cha halisi kuhusu Krismasi. Krismasi hata haikutajwa katika Biblia, kamwe hawakuiabudu siku ya kuzaliwa kwa Kristo. Hakukuwako na kitu kama hicho. Hilo ni fundisho la sharti la Katoliki ya Kirumi wala si fundisho la Kikristo, hakuna Maandiko kwake mahali popote katika Biblia na kwa miaka mia moja ya kwanza baada ya Biblia, unaona, hakuna lolote kuhusu hilo. Ni hadithi tu ya kubuni. Baba Krismasi, biashara, kila kitu, kitu hicho chote kimefungamanishwa katika upuuzi mtupu.

61-1217 -Ukristo Dhidi Ya Uabudu Sanamu

Natamani kweli kwamba watu wangeninii, wangeweza kufahamu katika ulimwengu huu, kwamba Krismasi ni nini hasa. Sasa, neno la kwanza Krismasi ni ninii—kwa namna fulani ni tamshi la Kikatoliki. Linamaanisha “Ya Kristo…” K-r-i-s-m-a-s-I, mnaona, “Misa ya Kristo,” mnaona. Ilitengwa ama ilianzishwa na kanisa la Kirumi. Naye Kristo katu hakuzaliwa tarehe ishirini na tano Desemba zaidi ya nilivyozaliwa mimi. A-ha. Ni mkusanyiko mtupu kabisa wa fundisho la sharti. Hivyo tu.

62-1216 -Kuporomoka Kwa Ulimwengu

Nao watu mitaani pamoja na viatu vyao vyenye visigino virefu, na wanajinyonganyonga huku na huko mitaani, wakikimbia madukani.

Na hapa hivi majuzi mke wangu alikuwa akiniambia, “Mtu fulani alisema, ‘Sijui kile nitakachomnunulia Baba.’ Kasema, “Ndugu yangu atamnunulia kwati la wiski, na huyo mwingine akasema atamnunulia shampeni.’ Na mmoja akasema, ‘Vema, nitamnunulia se—seti ya karata.’” Sherehe za Krismasi, upagani, ibada za ibilisi! Vema.

61-1217 -Ukristo Dhidi Ya Uabudu Sanamu

Leo nilikuwa nikifikiri juu ya makanisa makubwa yakipiga kengele, na kengele zikilia, na kadhalika namna hiyo; na watu wakienda kanisani, na kujitayarisha, na wanawake wakinunua kofia zao za Pasaka, na kadhalika. Jambo hili limefikia wapi? Jamani! Jinsi nisivyoweza kufahamu ambapo sungura ana uhusiano wo wote na ufufuo, unaona, (la, bwana) jinsi mti wa Krismasi ulivyo na uhusiano wo wote na Kristo. Ni upagani, rafiki zangu. Tumeacha njia mahali fulani. Hiyo ni kweli. Lakini sasa mwanamume aliyezaliwa mara ya pili ama mwanamke anatambua, kwa maana kuna uhai ndani yako, unaokwambia ya kwamba jambo hilo ni kosa. Hiyo ni kweli? [Kusanyiko linasema, “Amina.”—Mh.]

 53-0403 -Ukatili wa Dhambi, Na Adhabu Iliyogharimu Kuondoa Dhambi Maishani Mwetu

Angalieni, Hawa alikutana na wake. Na vivyo hivyo Hawa wa pili alikutana na wake huko Nikea, Rumi, ukalipa dhehebu, kanuni za imani, likakubali mafundisho ya sharti badala ya Neno; likashusha sanamu za kikafiri kama vile Jupita na kadhalika, na kuwainua Paulo na Barnaba. Na—na likashusha mungu-jua na mungu-mwezi, Ashtorethi, mungu-mwezi, pamoja na kosha ya duara juu yake, na kumfanya awe mama wa mungu-jua ambaye ni Jupita. Kisha likabadilisha siku ya kuzaliwa kwa Yesu kutoka Aprili, ambapo maumbile yote, ambapo alizaliwa chini ya kondoo dume, maana alikuwa kondoo dume, na likabadilisha hiyo ikawa siku ya kuzaliwa kwa mungu-jua katika jua kule, ambako inafanya siku moja…Kuna yapata tu tofauti ya dakika moja katika siku ambapo linapita kwenye tarehe ishirini na tano Desemba, siku ya kuzaliwa kwa mungu-jua, sio Mwana wa Mungu. Na kila mmoja wetu hujitumbuiza na Baba Krismasi, na kupamba miti, ukafiri, na mambo kama hayo, halafu ati tunajiita wenyewe Wakristo? Kanisa la Kikristo lina shida gani?

64-1212 -Wakati Wa Mavuno

6.     SANTA CLAUS ANACHUKUA UTUKUFU BADALA YESU KRISTO

Utangulizi

Santa Claus au “Father Christmas” ni upotoshaji wa Kidachi wa “Mtakatifu Nikolaas.” (“Mtakatifu Nicholas” alikuwa askofu wa Kikatoliki wa karne ya 4 wa Myra huko Asia Ndogo, aliyewapa watoto vitu; alitangazwa kuwa mtakatifu na Kanisa Katoliki, “akichukuliwa kama rafiki na mlinzi maalumu wa watoto.” Mavazi mekindu yanatokana na ukweli kwamba maaskofu na makadinali wa Kikatoliki nchini Italia huvaa nguo nyekundu.) Santa Claus pia alijulikana kama “Kriss Kringle,” ambayo ni ubadilishaji kutoka Kijerumani cha “Christ Kindl” – Mtoto Yesu.

Santa ni kufuru ndhidi ya Mungu kwa sababu ya kuwekwa kama mbadala wa Kristo! Mara kwa mara anapewa nguvu za Kimbinguni na sifa za Kiungu ambazo anayestahili ni MUNGU pekee. Fikiria. Anafanywa kuwa mjuzi wa kila jambo – anajua muda ambao kila mtoto analala, anaamka, amekuwa na afya mbaya au njema, na anajua hasa kila mtoto anachotaka (linganisha na Zaburi 139:1-4). Anafanywa kama kwamba yupo kila mahali – usiku mmoja tu wa mwaka anawatembelea watoto “wema” ulimwenguni kote na kuwaachia zawadi, anaonekana kuwa kila mahali wakati uleule. Pia anafanywa kuwa mwenye nguvu zote – ana uwezo wa kumpa kila mtoto kile anachotaka. Zaidi ya hayo, Santa Claus anafanywa kuwa mwamuzi mwenye mamlaka – hawajibiki kwa yeyote na hakuna mtu mwenye mamlaka zaidi yake, na anapokuja “mjini,” anakuja na mfuko wa zawadi kwa wale ambao tabia zao zimekubalika machoni pake.

Lakini hadithi ya Santa Claus inapotosha ukweli wa kuzaliwa kwa Kristo kwa kuchanganya kidogo ukweli na hadithi ya Santa Claus. Wazazi Wakristo wanapowadanganya watoto wao kuhusu Santa Claus, wanawaelekeza watoto wao mbali na Mungu na kuwasababishia kuzingatia mwanaume mnene mwenye mavazi mekundu mwenye sifa kama za mungu. Haya yote yanamfundisha mtoto kuamini kwamba, kama vile Santa, Mungu anaweza kuridhika na “matendo mema,” yaliyofanywa ili kupata kibali chake. Pia, wanafundisha kwamba haijalishi jinsi mtoto alivyokuwa mbaya, bado atapokea zawadi kutoka kwa Mungu – kama vile Santa hakuwahi kushindwa kuleta zawadi. Hata katika nyumba za Wakristo waaminifu, Santa Claus amaepachukua mahali pa Yesu kwenye uelewa na mapenzi ya watoto, akawa roho isiyopingika, alama, na kitovu cha Krismasi.

Hapa kuna baadhi ya nukuu kutoka kwenye mahubiri ya Ndg Branham kuhusu “Santa Claus”:

Ni kitu gani kilicho cha uwongo kuliko Baba Krismasi? Hapajawahi kuwa na kitu kama hicho. Kuwaambia watoto uongo, utawajibika kwake kwenye Siku ya Hukumu.

Si ajabu watu hawajui la kufanya. Wao ni…Wao—wao hawataki kabisa jambo lililo halisi. Watachukua kitu chochote bandia, bali hawataki kitu kilicho halisi. Hawazitaki zawadi za Mungu. Loo, jamani! Bila shaka. Hawamtaki Yesu, hilo ni jambo moja.

60-1225 -Zawadi Ya Mungu Iliyofungwa

Ni Krismasi. Mapambo yote, pilkapilka zote barabarani, za Baba Krismasi, hadithi ya kubuni ya Kijerumani, fundisho la sharti la Kikatoliki, hakuna hata sehemu moja yake iliyo kweli. Na inachukua mahali pa Yesu Kristo, katika mioyo ya Wamarekani wengi sana. Krismasi haimaanishi Baba Krismasi. Krismasi maana yake Kristo. Si mtu fulani aliye na kiko kinywani mwake, na akishuka kwenye dohani! Ukiwafundisha watoto wako vitu kama hivyo, unatarajia wakue wawe nini? Waambie Ukweli, sio kwenye hadithi fulani za uwongo. Waambie, “Kuna Mungu wa Mbinguni ambaye alimtuma Mwanawe, na hiyo ndiyo maana ya Krismasi. Naye yuko karibu kuja tena.”

58-1221M - Yuko Wapi, Mfalme Wa Wayahudi?

Ni wakati wa Krismasi, ondoeni hawa akina Baba Krismasi na kadhalika, tupilieni mbali upuuzi huo wa kibiashara. Ulisikia wapi kuhusu Baba Krismasi katika Biblia? Ni visasili vya Kirumi, havina maana hata kidogo, hakuna kitu kama hicho. Usiwafundishe watoto wako upuuzi kama huo.

64-1221 -Kwa Nini Ilibidi Iwe Ni Mchungaji Wa Kondoo

Kris Kringle yuko kote nchini. Alikuwa nani? Mjerumani, mtakatifu wa Kikatoliki miaka mingi iliyopita, mzee aliyeenda huku na huko akitenda mema. Na siku hizi imekuwa karibu ni ibada. Hiyo ni kweli. Ni sawa kuwaambia watoto, ama chochote unachotaka kufanya, nijuavyo mimi. Lakini jambo ni kwamba, ni rahisi sana kuanguka katika utaratibu huo upande mwingine, na kumsukumia Kristo nje, misingi halisi ya Kristo, ya Krismasi. Naye mtu anamchukua Kris Kringle badala ya Krismasi halisi, hiyo ni kweli, “Hakuna nafasi kwa ajili Yake katika nyumba ya wageni.”

49-1225 -Uungu Wa Yesu Kristo

Ninajua ya kwamba sisi watu hapa hatuwafundishi watoto wetu hadithi za uwongo kama za Baba Krismasi. Hatuamini katika kumwambia mtu yeyote uongo, kwa hiyo hamtawadaganya watoto wenu. Upuuzi kama huo, hicho ni hadithi ya uwongo katika upeo wake, kwa kitu kama hicho kupachukua mahali pa Kristo katika Krismasi.

Na Krismasi imepoteza…Krismasi si ibada tena; ni sherehe, kunywa, kucheza karata, karamu za ulevi, ukafiri mtupu tu. Na sio…Nami nilitaka kuninii…Labda baada ya Krismasi nitazungumza tena juu ya Krismasi, mnaona, kusudi isije ikawanyima watoto…Lakini huwezi kusema hilo kwa watoto wadogo jinsi hiyo. Hao huwaona jamaa wadogo usiku wa Krismasi wakipokea zawadi za Krismasi na kadhalika namna hiyo, hawalielewi. Mnaona? Wananinii tu…hao ni wadogo sana. Na inatupasa kuwakumbuka, kwamba wao…kwamba wana mambo shirika. Inatupasa kujishusha tupate kuwakumbuka hao jamaa wadogo.

61-1217 -Ukristo Dhidi Ya Uabudu Sanamu

SWALI: Vipi kuhusu mchezo wa Krismasi katika kanisa la Roho Mtakatifu?

Vema, kama ni kuhusu Kristo, huenda ikawa sawa. Lakini kama inahusu Baba Krismasi, simwamini huyo. Nimekwisha kuyaacha hayo. Siamini katika Baba Krismasi kamwe. Ona? Na baadhi ya hivi vitu vidogo vya Krismasi walivyo navyo, nadhani ni upuzi. Na…Lakini naona wamemwondoka kabisa Kristo katika Krismasi na kumweka Baba Krismasi mle.

59-1219 -Maswali na Majibu Juu ya Roho Mtakatifu

“Mtazamo sahihi kuhusu kusherehekea ‘msimu wa Krismasi’:”

Hebu nilifanye hili dhahiri. Siamini ya kwamba Yesu angejali ni siku gani uliiabudia siku ya kuzaliwa Kwake, kama ni tarehe 25, 26, ama kama ni Aprili, Mei, Juni, Julai, ama wakati wowote iwezao kuwa, mradi tu unaabudu, wewe mwabudu siku yoyote.

Lakini jambo ndilo hili. Wameuondoa utakatifu kutoka kwenye Krismasi, kuifanya siyo Krismasi bali, siku ya kuabudu, bali sherehe. Mnaona? Hatuninii…Mnawasikia watu wakisema, “Tutasherehekea Krismasi.” Hilo ni kosa. Kamwe hatupaswi kuisherehekea Krismasi. Krismasi ni siku ya kuabudu, sio sherehe.

61-1224 -Mabwana, Sisi Tunataka Kumwona Yesu

 Mungu awabariki. Sio hasa “Krismasi Njema,” bali baraka za Mungu za Krismasi ziwe juu yenu. Jalia Kristo wa Kalvari akufiche ndani Yake Mwenyewe, akufunike, akufunike sana na kukuvisha vazi la Neno Lake, mpaka Neno Lake litakapofanyika mwili ndani yako, ndilo ombi langu. Mungu awabariki.

61-1224 -Mabwana, Sisi Tunataka Kumwona Yesu

Mnapendana? Geukeni na kupeana mikono ninyi kwa ninyi, mseme, “Mungu akubariki. Kristo awe pamoja nawe.” Badala ya “Krismasi Njema,” mseme, “Kristo awe pamoja nawe,” mnapogeuka. Sasa usiondoke, ge—geuka tu, useme, “Kristo awe nawe.” (Kristo awe nawe.)

49-1225 -Uungu Wa Yesu Kristo

Kwenye mkesha huu wa Krismasi, Bwana, tunashukuru kwa ajili ya kipawa cha Mungu, kwa Mungu kutupa. Ingawa huu ni baadhi yake, kama tunavyoamini mioyoni mwetu, ushirikina fulani wa kikafiri wa siku ambayo wamejaribu kuitengeneza na kuifanya iwe kama misa ya Kristo, lakini sisi hatuji katika njia hiyo ya Baba Krismasi na miti ya Krismasi na mapambo. Bali tunakuja katika Jina la Bwana Yesu, kumwabudu Mungu wa Mbinguni, aliyefanyika mwili, mwili kama sisi, na akakaa miongoni mwetu, apate kutukomboa; na akapata dhihaka ya lile Jina, akapata dhihaka ya msalaba, akairuhusu taasisi ya kilimwengu kumwua Imanueli, kusudi Yeye aweze kutuletea Uzima wa Milele.

62-1223 -Dhihaka Kwa Sababu Ya Neno

Na utupe Roho, Roho wa kweli wa Krismasi. Wakati leo…kwamba wakati ambapo sherehe za kipagani, miti ya Krismasi inaabudiwa, hadithi za uongo za m—mtu anayeitwa Baba Krismasi, na sungura wetu wa Pasaka, na mitindo mbalimbali ambayo ulimwengu wa kibiashara umeitumia kwa faida yao, jalia iwekwe kando, Mungu. Jalia tuingie katika Kristo Neno, kwa kuwa tuliomba katika Jina Lake na kwa ajili ya utukufu Wake. Amina.

64-1221 -Kwa Nini Ilibidi Iwe Ni Mchungaji Wa Kondoo

WATU WENGI BILA KUJUA WANAVUNJA AMRI KUMI KWA KUSHEREHEKEA KRISMASI:

A: Usitamani – Watoto hujifunza kutamani zawadi za wengine, kutamani vitu vilivyo kwenye orodha ya Krismasi, kuwachosha wazazi wao kwa muda mrefu katika maduka ya vitu vya kuchezea, vyote kwa jina la “roho ya Krismasi.”

B: Usimshuhudie jirani yako uongo. – “Yesu ndiye sababu ya majira/msimu wa krismasi!”  ni kilio cha vita vya Wakristo wakati wa Krismasi,” ingawa ukweli ni kwamba hakuna msingi wa Kibiblia kwa sababu asili yake ni katika mifumo ya ibada za kipagani. Wakristo wengi wanawaambia uongo watoto wao kuhusu Santa Claus, “Baba Krismasi”, ambaye “injili” yake ni wokovu kwa njia ya matendo pamoja na kukubaliwa na thawavu isiyo na masharti. Wazazi huwadanganya watoto wao kwa miaka mingi kuhusu tabia kama ya Mungu ya Santa Claus, hali inayowataka kumwamini mungu wa uwongo na muongo, na kisha hawaelewi kwa nini baadaye watoto wao hawaamini na kutumaini katika Mungu wa kweli, Yesu Kristo.

C: Usiibe - Mienendo ya kutumia pesa wakati wa Krismasi kamwe haiwezi kustahimili mtihani wa utunzaji wa Biblia. Wakristo, wanapoadhimisha Krismasi, "wanaiiba" rasilimali za Bwana kwa kutozingatia matumizi sahihi. Wanatumia rasilimali hizi kwa wingi kwenye vitu visivyo na vya muhimu na visivyo na maana (mara nyingi) na kutokuwazingatia wale wanaohitaji, wakati huo huo wakidai kamwe hawana pesa za kutosha kununua vitabu vizuri vya Kikristo, kulipia ghalana za elimu ya nyumbani, au kununua Biblia kwa watoto wao. (Wakristo pia wangeweza kuwasaidia wale wenye mahitaji ya kiroho kwa kuwanunulia na kuwapa kanda, vitabu, n.k.) “Tunaiba” kutoka kwa familia zetu kile wanachohitaji na wanachostahili ili kuwanunulia zawadi wale wasiohitaji.

D: Usizini – Wakati huu “maalum” wa mwaka, mawazo yenye tamaa kwa kweli yanahimizwa. Vijana wanaruhusiwa kwenda kwenye karamu na kubaki nje hadi muda wa usiku, hivyo wanakutana na majaribu ambayo vinginevyo hayangekuwepo. Karamu ya Krismasi kwa watu wazima pia inachochea mawazo mabaya. Maeneo mengine, watu hutumia kofia zao kubadilishana funguo za vyumba vyao vya hoteli na kufanya vitengo vya kubadilishana wake. Uzinzi wa kiroho kwa kweli unahimizwa na “msimu” huu.

E: Usiue – Wivu na chuki kwa ndugu yangu (ambapo, kulingana na Mathayo 5, ni sawa na mauaji) kwa sababu ana zaidi kuliko mimi au kwa sababu anapokea zawadi kubwa ya Krismasi kuliko mimi. Hali hii hutokea sana wakati wa Krismasi ambapo watu wanadhihirisha ubinafsi, kiburi na tamaa zao.

F: Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako. – Kutoa zawadi za Krismasi si heshima kwa wazazi; neno “kubadilishana” zawadi (kutoa kwa kutarajia kupokea pia) ni ishara wazi ya dhihaka zinazoambatana na utamaduni huu.

G: Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Ikiwa siku ya Krismasi itakuwa Jumapili, makanisa mengi hurekebisha Siku ya Bwana ya ibada ili kuenanda na ratiba za watu, mara nyingi kwa kufuta ibaada ya kawaida ya Jumapili jioni. Wengi wa washiriks wake huwa na shughuli nyingi au wanakuwa wamechoka sana kuhudhuria ibada.

H: Usilitaje bure jina la BWANA, Mungu wako, maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure. “Kristo” na “misa” ni maneno mawili yanayopingana kabisa. Kuyaunganisha yote mawili ni kumkufuru Kristo. Kuchukua sherehe ya kipagani, kuifanya kuwa ya Kikristo, na kuiita sherehe ya kuzaliwa kwa Kristo, bila shaka ni kulitaja bure Jina la Bwana. Zaidi ya hayo, baadhi ya Wakristo wanaojitangaza hutumia dini (“Siku ya Kuzaliwa kwa Kristo”) kama kificho cha kufunika uovu wa tamaa ya kujilimbikizia, sanamu, choyo, uchafu, n.k. — sababu zote ni kutoa nafasi kwa matendo maovu.

I: Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia - Miti ya Krismasi, Mashada, Taa… watu wanatilia maanani hizi “picha” wakati wa Krismasi na kuvunja amri hii. Mungu ametupa “Neno” lake, sio sanamu za kumuabudu (1 Pet. 1:23; Kumb. 4:12, 15-19).

J: Usiwe na miungu mingine ila mimi. Kutafuta furaha ya kidunia, furaha, na utimilifu kupitia msimu wa Krismasi kwa Baba Krismasi badala ya uhusiano safi, wa kibinafsi, na wa Kibiblia na Yesu Kristo, ni dhahiri na rahisi "ibada ya sanamu".

 Pakua Pdf hapa